Tuesday, 10 May 2016
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba amesema uhaba wa sukari uliopo kwa sasa nchini umesababishwa na Rais
Pia Prof. Lipumba amesema hakuna sheria inayoruhusu Serikali au Bodi ya Sukari kupanga bei ya sukari nchini hivyo ametaka siasa kuacha kutumika katika mambo serious na wafanyabiasahara wasitishwe.
Swala la Sukari lisitu sahaulishe Lugumi na Ripoti ya CAG..... tusiwe wepesi wakutolewa kwenye Reli, Lugumi na Ripoti ya CAG imeishia wapi ama inaendeleaje?
Hivi ile kamati ya PAC imeishia wapi na ishu ya Lugumi? Mbona hapa pako
kimya? Na tukizingatia ni ishu inayogusa jeshi letu la polisi? Hapa jipu
halitumbuliki?
Nimejiuliza maswali hayo nikasema nilini Watanzania tutalazimisha Watawala wajue tumechoka na kusikia ishu zikiibuliwa na kuishia njia.... Au huko Bungeni wanaliongelea na sisi huku hatusikii wala kuona kwakuwa Bunge halipo live?
Swala la Sukari lisitu sahaulishe Lugumi na Ripoti ya CAG..... tusiwe wepesi wakutolewa kwenye Reli, Lugumi na Ripoti ya CAG imeishia wapi ama inaendeleaje?
HUU MCHEZO HAUHITAJI HASIRA
By Henry Kilewo
Nimejiuliza maswali hayo nikasema nilini Watanzania tutalazimisha Watawala wajue tumechoka na kusikia ishu zikiibuliwa na kuishia njia.... Au huko Bungeni wanaliongelea na sisi huku hatusikii wala kuona kwakuwa Bunge halipo live?
Swala la Sukari lisitu sahaulishe Lugumi na Ripoti ya CAG..... tusiwe wepesi wakutolewa kwenye Reli, Lugumi na Ripoti ya CAG imeishia wapi ama inaendeleaje?
HUU MCHEZO HAUHITAJI HASIRA
By Henry Kilewo
Wizkid azidi kung’ara duniani BILLBOARD HOT 100 TOP 10 awa no1 kwa Drake feat. Kyla & WizKid – “One Dance”
Wimbo ‘One Dance’ wa Drake aliomshirikisha msanii huyo wa Nigeria umekamata nafasi ya kwanza kwenye chati za Billboard Hot 100. Wimbo huo upo kwenye album ya Drake, Views ambayo pia nayo imeshika nafasi ya kwanza kwenye Billboard 200 chart.
BILLBOARD HOT 100 TOP 10
1. Drake feat. Kyla & WizKid – “One Dance”
2. Desiigner – “Panda”
3. Lukas Graham – “7 Years”
4. Mike Posner – “I Took a Pill in Ibiza”
5. Fifth Harmony feat. Ty Dolla $ign – “Work from Home”
6. Rihanna feat. Drake – “Work”
7. The Chainsmokers feat. Daya – “Don’t Let Me Down”
8. Zayn – “Pillowtalk”
9. Calvin Harris feat. Rihanna – “This is What You Came For”
10. Justin Bieber – “Love Yourself”

Monday, 9 May 2016
sukari tani 133 za sukari iliyoingizwa kimagendo yagawiwa bure
Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) imegawa Sukari yote ya Magendo Mifuko 5,319 yenye thamani ya Zaidi ya Shilingi Milioni 373.5 kwa Taasisi mbali mbali Mkoani Lindi baada ya kuthibitishwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA kuwa ni Salama kwa matumizi.
Sukari hiyo ilikamatwa mwezi Februari mwaka huu katika bandari ya Lindi ndani ya meli ya MV Hassanat ikiingizwa kinyume cha Sheria ikitokea nchini Brazil kupitia Zanzibar.
Sukari hiyo ilipaswa kulipiwa Kodi zaidi ya shilingi Milioni 246.
Sukari hiyo imegawiwa kwa taasisi 31 mkoani humo baada ya TFDA kuthibitisha kuwa sukari iko salama kwa matumizi ya binadamu.
Akizungumza wakati wa ugawaji wa sukari hiyo Mkurugenzi wa huduma na Elimu kwa mlipakodi TRA Richard Kayombo amesema baada ya kukamatwa kwa bidhaa hizo TRA kwa kushirikiana na taasisi nyingine za serikali ikiwemo ofisi ya mkuu wa mkoa wa Lindi, iliamriwa sukari hiyo kuigawa kwa watu wenye uhitaji katika mkoa huo zikiwemo taasisi za elimu, Afya, kambi za wazee na Jeshi la magereza.
Chanzo: TBC
rais magufuli awagomea wabunge nyongeza ya mikopo ya magari

Baada ya kuchaguliwa, wabunge walipatiwa milioni 90 za mkopo kwa ajili ya ununuzi wa magari, lakini baadhi yao walieleza kutoridhishwa na kiasi hicho, wakidai hakitoshelezi na kutaka kiongezwe hadi sh. milioni 120.
Taarifa za kuaminika zinaeleza kuwa wabunge waliwasilisha ombi kwa Rais Magufuli kuongezwa fedha lakini ombi hilo limekataliwa.
Chanzo cha kuamini kimedokeza kuwa mmoja wa wabunge wa CCM alimkumbushia Rais Magufuli ombi hilo wakati wa kikao cha chakula cha jioni, kilichofanyika wiki iliyopita mjini Dodoma.
Chanzo hicho kilieleza kuwa Rais Magufuli alikataa kuwaongezea wabunge fungu hilo kwa madai kuwa serikali yake haina fedha.
Kilieleza pia kuwa Rais Magufuli alikataa kuongeza fungu la mfuko wa jimbo kwa kuwa serikali haina fedha huku akiwataka wabunge kufanya kazi kwa bidii.
"Rais alisema kwa sasa hali si nzuri, amekumbana na changamoto mbalimbali na kutuahidi kulichukua ombi letu, endapo hali itatengemaa atatuangalia kwa sababu hata yeye analitambua hilo kwa sababu alikuwa mbunge."Kilisema chanzo hicho
floyd mayweather kurudi tena ulingoni
FLOYD MAYWEATHER na staa wa UFC, Conor McGregor wapo mbioni kuingia ulingoni kuzichapa kwenye pambano kubwa na aghali zaidi la masumbwi katika historia.
Gazeti la The Sun limedai kuwa Mayweather, anatarajia kuzichapa na staa huyo jijini Las Vegas mwaka huu.
Mayweather alitangaza kustaafu ndondi akiwa ameshinda mapambano yote 49 aliyowahi kupigana. Kwenye pambano hilo Mayweather atachukua paundi milioni 100 huku McGregor atachukua paundi milioni 7.
Tangazo rasmi litatolewa wiki chache zijazo.
Chanzo kililiambia gazeti la The Sun kuwa Floyd alichukia baada ya Conor kudai anaweza kumtwanga KO ndani ya sekunde 30 tu na sasa anataka kumuonesha kazi.
Gazeti la The Sun limedai kuwa Mayweather, anatarajia kuzichapa na staa huyo jijini Las Vegas mwaka huu.
Mayweather alitangaza kustaafu ndondi akiwa ameshinda mapambano yote 49 aliyowahi kupigana. Kwenye pambano hilo Mayweather atachukua paundi milioni 100 huku McGregor atachukua paundi milioni 7.
Tangazo rasmi litatolewa wiki chache zijazo.
Chanzo kililiambia gazeti la The Sun kuwa Floyd alichukia baada ya Conor kudai anaweza kumtwanga KO ndani ya sekunde 30 tu na sasa anataka kumuonesha kazi.
soma habari zilizopo katika magazeti yaleo tarehe 9
Subscribe to:
Posts (Atom)